UNYANG'ANYI WA KUTUMIA SILAHA WAMFIKISHA MAHAKAMANI WILAYANI SENGEREMA


Mtu   mmoja  amefikishwa   katika   mahakama   ya   wilaya  ya  Sengerema    mkoani   mwanza    kwa  tuhuma   ya  unyangh’anyi  wa kutumia  silaha.

Akisoma  shitaka  linalomkabili   mbele  ya  hakimu  wa  mahakama  hiyo  BI  MONIKA   NDYEKOBORA  ,mwendesha  mashitaka   wa  jeshi  la  polisi  INSPECTA  MARTHA  SLIVESTA  ,amemtaja   mshitakiwa   kuwa  ni  ISACKA GELARDI   mwenye   umri   wa  miaka   28 mkazi   wa  KATWE  wilayani  hapa.

INSPECTA  MARTHA  amesema  kuwa  mshitakiwa  anashitakiwa  kwa  kosa  la tuhuma   ya  unyangh’anyi  wa kutumia  silaha  kinyume  na  kifungu  namba  287  A cha   kanuni  ya  adhabu  sura  ya   16,  kuwa  mnamo   januari 18 mwaka   huu  majira  ya  saa  8:00  usiku  huko  katika kijiji  cha  katwe  wilayani   sengerema  mkoani  mwanza aliiba  pesa   tathilimu   shilingi   elfu   hamsini  simu   1   aina  ya   Aitel    yenye   thamani   ya  shilingi   elfu  ishilini  na  nne  na  jumla  ya   mali   yote   ni   shilingi  elfu   sabini  na  nne   mali   ya  NDALO  SAGATI.

Hata  hivyo  mshitakiwa  amekana  kutenda  kosa  hilo  na  mshitakiwa amerudishwa  rumande  kwa    hadi  februari  15   mwaka  huu  kesi  hiyo   itatajwa  kwa  maelezo   ya  awali  mahakamani  hapo.
Na Joyce Rollingstone.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.