WAZAZI WAMEWEKA MIKAKATI YA KUDHIBITI UTORO WA WANAFUNZI SHULENI WILAYANI SENGEREMA


Wananchi wa  Kijiji   cha Kijuka  kata ya Nyamazugo wilayani Sengerema mkoani Mwanza wameweka   mikakati  ya  kudhibiti utoro wa wanafunzi shuleni  ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua kali wazazi ambao watoto wao hawatahudhuria shuleni.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa kijiji cha kijuka Bw, Sospeter  Lusapa Dotto alipoongea na Radio Sengerema ofisini kwake.

Mwenyekiti amewataka wazazi kutowazuia watoto kwenda shule na kuwaomba kutoa ushirikiano ili kuhakikisha wanafunzi wanatumia vyema fursa ya serikali ya elimu bure na kuinua kiwango cha ufaulu.


Aidha amebainisha changamoto ya upungufu wa madawati iliyopo shuleni hapo  na  kuwataka wananchi kuweka utaribu wa kuchangia ili kumaliza kero hiyo.


Mwenyekiti  amewataka wazazi na walezi kuwa makini na watoto ili kuwajengea uwezo na ufaulu mzuri pasipokuwa na visingizio vya utoro kitendo ambacho  kinadidimisha  kiwango cha elimu  shuleni hapo .   
 Na Charles Sungura.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.