WANAHABARI NCHINI WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI NA WELEDI WA TAALUMA YAO


Waandishi wa habari nchini wametakiwa kuzingatia maadili na weledi wa taaluma yao katika utendaji kazi ili kukuza taaluma.
Hayo yamesemwa na mkufunzi wa mafunzo yakuandika habari kwa waandishi wa habari za vijijini BI ROSE HAJI MWALIMU yanayoendelea katika Ukumbi wa Wakala Wa Majengo mkoani DODOMA.



Amesema waandishi wa habari wanatakiwa kutokwenda kinyume na maadili kwa kuandika taarifa za ukweli, pamoja na kutumia vyanzo vinavyoaminika kwa kuzingatia kanuni na taratibu za uandishi wa habari.
Akichangia mada hiyo mmoja wa washiriki katika warsha hiyo MATHIAS TOOKO amesema endapo waandishi wa habari watazingatia waliyofundishwa wataleta ufanisi  na kuongeza uaminifu na mvuto kwa wasikilizaji.
Mafunzo hayo ya siku nane yanayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni –UNESCO- yatahitimishwa tarehe 13 mwezi wa pili kwa maadhimisho Siku ya Redio Duniani.




Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.