WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA WALALAMIKIA KUTOPEWA DAWA YA KUNYUNYUZIA ZAO HILO MKOANI GEITA


Zaidi   ya   wakulima    300   wa   zao   la  Pamba katika kijiji cha  Ndelema   Kata ya  Kamena   Mkoani  Geita  wameandamana hadi  kwenye ofisi  ya afisa mtendaji wa kijiji hicho  wakilalamikia  kutopewa  dawa ya kunyunyuzia  Pamba  inayokidhi mahitaji  ya wakulima.                                        
 Image result for PICHA YA ZAO LA PAMBA
Maandamano hayo ya wakulima yamekuja kutokana na bodi ya Pamba  kuwaletea  chupa  35  pekee za dawa    ili  hali   wakulima  wa  zao hilo     wako zaidi ya  300 katika kijiji  hicho ,huku mazao yao yakiendelea kushambulia na wadudu shambani.          



Naye   Mhasibu   wa  Kijiji  hicho   Bwn. Malimi Lushinge    katika hali ya kushangaza   amewambia  wakulima  hao  hajui  ni lini   bodi ya pamba itawaletea dawa  hizo , huku akilazimika kuwaonyesha   stakabadhi ya chupa 35 za  dawa   zilizopo.          
  

Kwa upande    wake   Afisa  Mtendaji  wa  kijiji  hicho   Bwn, John Kahindi  amesema kuwa  mamalamiko ya  wakulima hao ni ya msingi   kwa kuwa dawa iliyoletwa  haikidhi mahitaji ya wakulima   na kuweka wazi kuwa  tayari amawasiliana na afisa kilimo   ngazi  ya  kata    ili  kupata  ufumbuzi  wa  tatizo hilo.

Maandamano  ya  Wakulima  wa pamba  katika kijiji cha  Ndelema  kulalamikia  kupewa dawa ya kunyunyizia  zao la pamba    yamesababisha    wasitishe  shughuli  zao kwa   kwa siku nzima.

Na Emmanuel Twimanye.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.