SERIKALI YAWAONDOA HOFU WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA SENGEREMA JUU YA UPATIKANAJI WA DAWA


Kutokana na   Wakulima  wa  zao  la  Pamba   wilayani  Sengerema kufanikiwa  kuvuka  lengo  la kulima zao  hilo Serikali  imewaondoa wasiwasi kuhusiana na upatikanaji wa   dawa.

Image result for PICHA YA ZAO LA PAMBA
Akizungumza na Radio Sengerema Mkuu wa wilaya ya Sengerema Mh.Emmanuel Kipole amesema kuwa,wananchi wameonesha mwitikio mkubwa baada ya kuhamasishwa na serikali  ,hali iliyopelekea wavuke lengo kutoka hekari elfu 28 walizotarajia  zilimwe   hadi  kufikia  ekari  Elfu 44.

Aidha,Mh.Kipole amewaondoa hofu wakulima kuhusiana na tatizo la uhaba wa dawa na kuahidi kuwa itapatikana, kwani wanaendelea kufanya jitihada ili kukamilisha upatikanaji wake.  

Hata hivyo,wakulima  wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa dawa, hali ambayo imezua hofu kubwa  miongoni mwa  wakulima   ikiwemo      kuharibiwa   kwa kushambuliwa  na wadudu   mazao yao katika  mashamba  yao  
 Na,MICHAEL MGOZI   

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.