MOTO MKUBWA WATEKETEZA BWENI LA WAVULANA SHULE YA SEKONDARI KATUNGURU SENGEREMA


Moto mkubwa umezuka na kuteketeza   bweni la wavulana katika shule ya Sekondari Katunguru iliyopo wilayani Sengerema mkoani Mwanza huku chanzo chake kikiwa hakifahamiki.

Hayo yamethibitishwa na mkuu wa shule hiyo Mwalimu Baraka Ezekiel Msimba ambapo amesema moto huo umetekeza vitu vyote vilivyokuwa ndani ya bweni hilo huku wanafunzi   takribani 5 wakinusurika kifo.


Kufuatia ajali hiyo mkuu wa Mkoa wa Mwanza  John Mongella ametoa pole kwa wahanga wa tukio hilo huku akiahidi kuchangia akiahidi kuchangia magodoro 50 mifuko 50 ya saruji.

 
Mkuu wa mkoa ameagiza kuanza ujenzi wa mabweni hayo mara moja.

Nao wanafunzi wameeleza kwa masikitiko makubwa huku wakidai kuwa  ajali hiyo hawajui imetokana na nini kwani wao walikuwa darasani wakijisomea.















Hata hivyo mkuu wa wilaya ya Sengerema amewataka wanafunzi kusoma kwa bidii licha ya kukumbwa na ajali hiyo.

Na Tumain John.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.