MKUTANO WA KIJIJI WASABABISHA KUSIMAMA KWA SHUGHULI ZA UCHENJUAJI WA MADINI YA DHAHABU MKOANI GEITA


Mkutano wa serikali ya Kijiji cha Mawemeru kata ya Nyarugusu wilayani Geita,umezuia shughuli za uchenjuaji wa Madini ya Dhahabu zinazofanywa na Mgodi wa Plas uliopo katika Kitongoji cha Mgombani,kutokana na Mgodi huo kuwa kwenye makazi ya watu.
 Image result for PICHA YA MADINI YA DHAHABU MGODINI
Mkutano huo wa dharula umekutana baada ya Kupokea Malalamiko ya Wananchi wanaoishi jrani na Mgodi huo wakihofia maisha yao kutokana na kemikali zinazotumika kuchataka madini hayo.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mawemeru Mlindwa Maganga akatoa Ufafanuzi na baadaye Kaimu Mtendaji akasoma Taarifa ya wakazi wa Kitongoji cha Mgombani.


Wakazi wa Kitongoji cha Mgombani wahofia Maisha yao hasa kwa watoto wao kutokana na Uwepo wa Mgodi huo,kwani sumu inayotumika ni hatari kwa viumbe hai.

Mwenyekiiti wa Wafugaji kata ya Nyarugusu Selestine Hechimubi amesema Shughuli hizo zinahatarisha Viumbe hai Vingine wakiwemo mifugo.

Aidha,Diwani wa Kata ya Nyarugusu Swalehe Juma amebariki maamzi ya Mkutano huo na kumtaka Mwekezaji kama hakuridhia uamzi huo kukata rufaa ngazi nyingine.

Meneja wa Mgodi huo Aulice Mtegeta amesema Uongozi wa Mgodi umepokea kwa masikitiko Makubwa maamzi ya Mkutano huo.


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.