MBUNGE WA JIMBO LA SENGEREMA AKABIDHI MIFUKO 200 YA SARUJI KATIKA SHULE YA SEKONDARI KATUNGURU




Moto mkubwa uliozuka na kuteketeza   bweni la wavulana katika shule ya Sekondari Katunguru iliyopo wilayani Sengerema mkoani Mwanza usiku wa kuamkia februari 07 mwaka huku chanzo chake kikiwa hakifahamiki hatimaye Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mh William Mganga Ngeleja akiwakilishwa na Diwani wa Kata ya Katunguru Mh Methew Lubongeja amekabidhi mifuko 200 ya saruji.



Image may contain: 17 people, people smiling, outdoor
Diwani wa Kata ya Katunguru Mh,Methew Lubongeja (Kushoto) akikabidhi mifuko 200 ya Saruji kwa mkuu wa shule ya Sekondari Katunguru Mwalimu Baraka Ezekiel Msimba (kulia)

Diwani Mathew Lubongeja akiongea na jumuiya ya wanafunzi wa Katunguru Sekondari baada ya kukabidhi mifuko 200 ya saruji iliyotolewa na Mh mbunge William Mganga   Ngeleja kwa ajili ya ujenzi mpya wa bweni lilioungua na moto .





Image may contain: 4 people, people smiling, outdoor


Diwani Mathew Lubongeja amemuwakilisha mh William Ngeleja kutoa mifuko ya saruji 200 kuchangia kujenga bweni jipya baada ya bweni la awali kuungua moto katika Shule ya Sekondari Katunguru,

Mkuu wa shule hiyo Mwalimu Baraka Ezekiel Msimba amemshukuru mh Mbunge wa Jimbo la Sengerema kwa msaada  alioutoa kwa wakati huu mgumu wa majonzi.

Na Veronica  Martine.



Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.