JUMLA YA MITI 132 YAOTESHWA KATA YA IBISABAGENI WILAYANI SENGEREMA


Jumla ya miche mia moja thelathni na mbili(132) ya miti imepandwa kwenye eneo la  stendi  ya   mtaa wa Ibisabageni kata ya Ibisabageni wilayani Sengerema kwa lengo la kuenzi kauli ya kuboresha  mazingira kwa nchi nzima.

Miche hiyo imepandwa  katika  uzinduzi wa upandaji miti  uliofanyika katika  kata ya Ibisabageni wilayani hapa ambapo Zoezi hilo  limeongonzwa na mkuu wa wilaya ya Sengerema Mh. EMMANUEL ENOCK KIPOLE.








Mh. Kipole amewapongeza  wananchi wa mtaa huo kwa kuonyesha jitihada kubwa  za kuchangia pesa kiasi cha shilingi   mia mbili kwa kila mwananchi  kwa ajili ya upatikanaji wa miti hiyo. 

Kwa upande wao  baadhii ya wananchi wa mtaa huo  wamemshukuru  mkuu wa Wilaya kwa kuzindua zoezi hilo kwani miti ni muhimu   katika kutunza mazingira .  

Sanjari na hayo mkuu huyo wa wilaya amewaagiza mwenyekiti wa mtaa  pamoja na  Afisa  mtendaji  wa kata  hiyo  kuwa  mstari wa mbele   kuimarisha   ulinzi wa   rasilimali  hizo    ili  zisiharibiwe    na  mifugo .
Na Esther Mabula

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.