HUDUMA YA MAJI YATARAJIWA KUREJESHWA SAA TANO USIKU FEB 08 WILAYANI SENGEREMA


Huduma  ya maji Wilayani Sengerema  Mkoani  Mwanza   inatarajiwa  kurejea     katika  hali yake  ya  kawaida  usiku wa leo majira ya saa  tano     na kumaliza usumbufu kwa  wananchi  wa  kusaka  maji umbali mrefu  na kutumia maji ya kwenye mifereji yasiyo safi  na  Salama. 


Neema hiyo  imetangazwa na Mkurugenzi  mtendaji wa Halamsahauri  ya  Wilaya ya Sengerema  Bwn, Magessa Mafuru Boniphace  wakati akizungumza na Radio  Sengerema kwa njia ya simu   akiwa  Mjini  Dodoma  ambapo   amesema   kuwa  wakazi wa Sengerema wasubiri neema hiyo usiku  wa leo  huduma hiyo muhimu    kwa shauku    kubwa   na kwamba kwa sasa katika chanzo cha maji cha Nyamazugo  Wilayani Sebngerema  wameanza  kuruhusu maji  kwa ajili ya kujaza matenki ya maji na kisha usiku watayaruhusu ili  yawafikia wananchi.  
       
Aidha Bwn, Boniphace katika kutambua umuhimu wa wananchi wa halmashauri yake   amewaomba radhi   kwa usumbufu walioupata kwa siku 24   toka lilipotokea katizo la maji katika mji wa Sengerema huku  akiwaomba wananchi waendelee kulipa bili ya jai kuepusha  kujitokeza tena  katizo hilo la maji mara kwa mara .
Na Emmanuel Twimanye 

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.