ZAIDI YA KAYA 250 KATI YA 500 HAZINA VYOO KITONGOJI CHA MSIKITINI HALMASHAURI YA BUCHOSA

Zaidi ya kaya 250 kati ya 500 hazina vyoo katika kitongoji cha Msikitini kilichopo katika kijiji cha Kanyara kata ya Bulyaheke Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema Mkoani Mwanza.

Image result for PICHA YA CHOO CHA KIJIJINI
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara Mwenyekiti wa kitongoji hicho Samola Makubi amesema kaya nyingi zina kabiliwa na ukosefu wa vyoo ambapo kati ya kaya 5 kaya 3 zimekuwa hazina vyoo hali ambayo hulazimu kujisaidia ovyo.

Kufuatia hali hiyo Mwenyekiti huyo imemlazimu kutoa siku 6 kwa  kaya hizo  kuhakikisha zinakuwa na vyoo vyinginevyo msako mkali utaanza kwa wale watakao kaidi agizo hilo.

Baada ya mkutano huo kuahirishwa wananchi wakaunga mkono agizo la mwenyekiti huyo.

Kitongoji cha Msikitini licha ya kukabiliwa na ukosefu wa vyoo lakini ni miongoni mwa vitongoji vikubwa  vilivyoko katika kijiji cha Kanyara ambacho kina kadiliwa kuwa na kaya 500 na jumla ya wakaazi wapatao alfu nane (8000) hali ambayo hulazimu kujisaidia kwa kuchangia vyoo kwa kaya jirani wengine wakilazimika kutumia mifuko ya lambo kujisaidia huku wengine wakijisaidia katika fukwe za ziwa Victoria.


KATEMI LENATUS.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.