WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI ISACK KAMWELE AMUBADILIKIA MHANDISI WA MAJI MKOA WA MWANZA ATAKA UKWELI JUU YA KUTOKAMILIKA KWA MRADI WA MAJI BUCHOSA.

Waziri wa maji na umwagiliaji Eng, Isack Kamwele amemuagiza mhandisi wa maji mkoa wa mwanza kupeleka watalamu katika miradi ya maji iliyopo katika halmashauri ya Buchosa  ilikubaini sababu zinazo pelekea miradi hiyo kuto kukamilika kwa wakati.
Image result for picha ya waziri wa maji na umwagiliaji isack kamwela
Eng, Kamwele ametoa agizo hilo baada ya kutembelea mradi wa maji wa luchili na Lumeya ambapo amebaini miradi hiyo hadi sasa imekwisha tumia  asilimia 5 ya fedha huku fedha zingine zikiwa hazijatumika.
Hata hivyo ameshangazwa na utata uliopo kwa halmashauri za Sengerema na buchosa kushindwa kuweka wazi makabidhiano ya miradi hiyo  ambapo halmashauri ya buchosa imedai kuto  kabidhiwa miradi kutoka halmashauri ya Sengerema ili hali halmashauri ya Sengerema ikikili kukabidhi miradi hiyo katika halmashauri ya buchosa.
Awali akikagua miradi hiyo ameipongeza halmashauri ya Sengerema kwa kukamilisha mradi wa maji wa Nyamazugo kwa asilimia 100,ambapo amesema amefurahishwa na hatua hiyo kwani tayari wananchi wa Sengerema wananufaika na mradi huo.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya Sengerema Mh Emmanuel Kipole amemhakikishia waziri wa maji kuhakikisha anachukua hatua kwa mkurugenzi atakaye baina kuidanganya ofisi ya mkuu wa wilaya, kuwa tayari makabidhiano yalishaa fanyika kwa halmashauri hizo.
Image result for mkuu wa wilaya ya sengerema emmanuel kipole
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm wilaya ya Sengerema Bwana Mac Agustine Makoye ameitaka serikali kuchukua hatua za haraka kubaini ugumu wa kuto kukabidhiana miradi kwa halmashauri hizo kwani kufanya hivyo ni kukwamisha ilani ya ccm ya mwaka 2015.

Na Katemi Lenatus.



Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.