WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AKABIDHI SH,MILION 20 KWA AJILI YA KUKAMILISHA MRADI WA MAJI

Waziri wa maji na umwagiliaji  Mhandisi Isack Kamwele amekabidhi kiasi cha shilingi milioni 20 kwa ajili ya mradi wa maji  katika mtaa wa Bukala kata ya Ibisabageni  wilayani Sengerema mkoani Mwanza.

Akizungumza katika mkutano wa wananchi na viongozi wakati akikabidhi mabomba hayo , katika mtaa wa Bukala  amesema kuwa wananchi washirikiane pamoja na viongozi ili kuweza kupata maji safi na salaama na kutoa agizo kuwa  ndani ya wiki tatu maji yawe yamepatikana.



Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Sengerema  mh.Emmanuel Kipole amesema kuwa wananchi wanatakiwa kutumia nguvu kazi ili kuhakikisha zoezi la  upatikanaji wa maji linakamilika mapema na kuondokana na changamoto hiyo .
Image result for PICHA YA mkuu wa wilaya ya sengerema emmanuel kipole

Mh .kipole ameongeza kwa kusema kuwa wanafanya jitihada za upatikanaji wa maji katika maeneo mbalimbali ili kusaidia wananchi na kuunga mkono kauli ya mh. Rais wa awamu ya tano  Dkt .John Pombe Magufuli ya kumtua ndoo ya maji mama.



Pia wananchi wamemshukuru waziri  wa maji na umwagiliaji mhandisi  kamwele  na kusema kuwa, tatizo la maji limekuwa likiwasumbua kwa muda mrefu hivyo wamepokea mabomba hayo kwa furaha .
Na Glorius Balele.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.