WANANCHI WAHIMIZWA KUTUNZA MAHINDI WALIYOYAVUNA ILI KUJIKIGA NA BAA LA NJAA WILAYANI SENGEREMA

Wananchi  wa  mtaa  wa  Kilabela   kata  ya  Mwabaluhi   wilaya  ya  Sengerema,  Mkoani Mwanza   wametakiwa  kutunza   Mahindi  Waliyoanza  kuyavuna kwenye mashamba yao     ili kujikinga na baa la njaa katika siku za usoni. 
      Image result for PICHA YA MAHINDI
Akizungumza  na  Redio  Sengerema  Ofisini  kwake  januari 5  mwaka  huu, mwenyekiti  wa  mtaa  huo  Bwn,  Samweli  Macheni  Nzungu,  amekemea  kitendo  cha  wananchi  kusahau shida  ya  uhaba   wa   chakula iliyokuwa   ikiwakabili   na  badala  yake  wameanza  kuuza  chakula,  hali  ambayo bila  kuikomesha   kwa sasa   huenda  ikasababisha     njaa  hapo   badae.

 Mwenyekiti  Nzungu   amesikitishwa   na kitendo  cha baadhi ya  wananchi   kuuza   chakula    na   kusema   kuwa,   wananchi  wanatakiwa  kukumbuka  hali  waliyokuwa  nayo  hapo awali  ,huku  akionya   mtu yeyote  atakayeonekana   na  mahindi  mabichi  akamatwe  na  uchunguzi  ufanyike  ikiwemo  kuonana  na  alieuza  mahindi  hayo kwa   hatua zaidi za kisheria.


Aidha  Bwn ,Macheni  amelaani  vikali   kitendo    cha  kukata  mahindi  mabichi  na  kwenda  kuuza  kwa  wachomaji,  na kuwataka  waache  tabia  hiyo, kwa madai  kuwa  hali hiyo    inaweza  kusababisha  watu  kuibiwa  mahindi  yao   pamoja na  kumaliza mahindi  yakiwa  mashambani  na kujutia   baadae.
Na Thobias Ngubila

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.