WANANCHI WA MTAA WA IBISABAGENI SENGEREMA WAADHIMIA KUPANDA MITI

Mwenyekiti  wa  mtaa  wa  Ibisabageni  kata  ya  Ibisabageni  wilayani  Sengerema, ameadhimia  kuboresha  mazingira  kwa  kupanda  miti  mtaani  hapo  ili  kuunga  mkono   kampeni    ya  serikali  ya  kutunza  mazingira nchini.

Image result for PICHA YA MITI ILIYOOTESHWA
Hayo  yamebainishwa  na  mwenyekiti  wa  mtaa  huo  Bwn,  Stanle  Felix,  katika  kikao  cha  hadhara    mtaani  hapo,   chenye lengo  la   mipango  mikakati  ya maendeleo   ya  mtaa  huo  kwa  mwaka  2018.

Hata  hivyo Bwn,  Felix   amesema kuwa   kuwa  jukumu  la  kuchangisha  michango yoyote   ya maendeleo    kwa  wapangaji  libaki  kwa wamiliki  wa  nyumba  sambamba  na   kumuunga  mkono  kwa ajili  ya  upandaji   miti,  na  ujenzi  wa  ofisi  ya  mtaa.

Kwa upande  wao wananchi  katika   kikao  hicho   wameibua  baadhi ya  kero   kwa     baadhi  ya  wapangaji     ikiwemo     kutotoa  michango   pindi inapohitajika     kuchangia  katika   maendeleo  ya  mtaa  huo.


Katika  hatua  nyingine  mwenyekiti  huyo  amewahakikishia  wananchi  wake  kuwa  maendeleo  hayaji  bila  kuwa  na  mipangilio  na  mipango   mahususi, ikiwa  ni  pamoja  na  Machungu  ya  kufanya  kazi  kwa  bidii.

Na Thobias Ngubila.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.