VICHAKA VYAGEUKA KUWA VYOO KATIKA MNADA WA MIFUGO WA KAMENA MKOANI GEITA

Wananchi    wanaopeleka  mifugo  yao   kuuza   katika  Mnada wa Kamena   uliopo   katika  kata ya  Kamena Mkoani Geita  wanalazimika kujihifadhi  kwenye vichaka   kutokana na mnada huo kukabiliwa na ukosefu wa choo kwa  zaidi ya mika 43 bila kupatiwa ufumbuzi.



Radio Sengerema imezulu katika mnada huo na kujionea  idadi kubwa ya wananchi wamegeuza vichaka  kuwa choo hali ambayo itasababisha   wananchi hao kukumbwa  na magonjwa ya mlipuko katika kipindi  hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha.

Licha ya mnada huo  kuingiza  mapato mengi katika  halmashauri  ya Geita lakini hadi sasa  hakuna   huduma ya choo katika mnada huo.


Diwani  wa  kata ya Kamena   Mh,Peter Kulwa alipotafutwa na Radio  Sengerema kwa njia ya simu    amekata simu  kwa  madai kuwa yupo kwenye kikao hawezi  kulizungumzia jambo  hilo.



Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya  ya   Geita   All Kidwaka   ameahidi kulishughulikia suala la ujenzi  wa  huduma  ya choo katika mnada huo haraka  iliwezekanavyo  ili  kunusuru wananchi kujihifadhi kwenye    vichaka.   
Na Emmanuel Twimanye. 

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.