UPUNGUFU WA VIFAA WASABABISHA KUKWAMA ZOEZI LA UPIMAJI VIWANJA SENGEREMA

Upungufu  wa  vifaa   umepelekea  zoezi   la   upimaji     wa  viwanja  kuchelewa     katika   mtaa   wa   Kanyamwanza  kata  ya   Mwabaluhi   wilayani   Sengerema   mkoa   wa    Mwanza.
Related image

Akizungumza  katibu  wa  kamati  ya  upimaji  na  urasimishaji  wa  viwanja   katika mtaa huo  Bwn,Joseph  Maxmilian  Kayanda ameeleza upimaji  ulivyoanza  mtaani  hapo.


Katibu  huyo  amezungumzia  jitihada  wanazozifanya  kama  kamati  kuhakikisha  kampuni  ya  Geop  Geomatic Interprisess inaongeza   vifaa   ili  kukamilisha upimaji  kwa  wakati.


Hata  hivyo  Bwn,  kayanda  amekiri  kukumbana  na  changamoto  katika  zoezi  hilo   ikiwemo  uelewa mdogo wa  wananchi    juu  ya  hatimiliki inayatolewa sasa  na  Ofa zilizokuwa  zikitolewa  awali.

 Aidha  katibu  huyo  amewataka  wananchi  kutambua  umuhimu  wa  hatimiliki   na  kwamba  inaweza  kuwasaidia  katika  mambo mbalimbali  sambamba  na  kuwa  na  uhakika  wa  kumiliki  aridhi  kisheria.
Na Thobias Ngubila


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.