UKOSEFU WA ELIMU YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UMESABABISHA WANANCHI KUVAMIA MAPORI YA AKIBA MKOANI KAGERA

Ukosefu wa elimu juu ya utunzaji wa mazingira imepelekea baadhi ya  wananchi kuvamia katika mapori ya akiba kufanya shughuli za kijamii hali inayopelekea mapori hayo kukauka kwa vyanzo vya maji na kukosekana kwa mvua.



Kauli hiyo imetolewa na kaimu meneja wa wakala wa misitu Tanzania wilaya ya Muleba mkoani Kagera  Bw. Samwel Magina wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.


 Bw. Magina amesema kuwa wamekuwa wakiweka doria hususani katika hifadhi ya Ruhiga ambayo ndio imeathiriwa na shughuli za binadamu ikiwemo wananchi kukata miti ovyo na kuchoma mkaa.


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.