TANI 6 ZA SAMAKI WACHANGA ZAKAMATWA SENGEREMA.


Takribani  tani  6  za  samaki  aina   ya    Sangara    wenye     thamani ya  shilingi    milioni 24 na  nyavu    haramu  912 zenye  thamani ya  shilingi    milioni 22.8    zimekamatwa  kwenye  shamba  la  Bwn,Joseph Kando   maarufu  kama Njiwa Pori   katika kijiji cha  Kawekamo  kata  ya  Nyampande   Wilayani  Sengerema  Mkoani    Mwanza.   


Akithibitisha kukamatwa kwa  samaki  hao   kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya   ya Sengerema Mh,Emmanuel Kipole  Katibu Tawala wa Wilaya ya Sengerema   Bwn,Alen Agustine   amesema taarifa za uwepo  wa samaki hao  wamepewa na raia wema.







Kwa upande wake Kaimu Afisa uvuvi    wa Halmashauri ya  Sengerema   Bwn,  Benedictor  Magonda  amewaomba wananchi waendelee kutoa  ushirikaiano  ili watokomeze  uvuvi haramu  ndani ya Ziwa Victoria.
 

Na Veronica  Martine.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.