DIWANI AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUWA ATAIKARABATI BARABARA ITOKAYO IKINA KWENDA MUHAMA B MKOANI GEITA

Diwani wa kata ya Nyaruyeye   Mkoani Geita  Mh, Malimi Samson  amewahakikishia wakazi wa  Vijijiji vya  Muhama B, na  Ikina    kuwa  ataikarabati barabara  itokayo  Ikina  kwenda Muhama B,  hadi Nyarugusu  Mkoani  humo.  
Image result for picha za mkoa wa geita
      
Kauli  ya  Diwani huyo imekuja  kufuatia barabara hiyo  kuharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha  hali ambayo imepelekea  baadhi ya akinamama wajawazito kujifungulia njiani   kutokana na vyombo vya moto kushindwa kupita katika barabara   hiyo.

Ubovu  wa barabara hiyo umesababisha pia wagonjwa kuchelewa kufikishwa  kwenye matibabu kwa wakati na    wakulima kushindwa  kusafirisha  mazao yao  sokoni kwa ajili ya  kujipatia kipato  cha  kuendesha familia zao.


Hata hivyo   mwaka 2018   ni     wakati    muafaka kwa viongozi waliochaguliwa na wananchi  ikiwemo  madiwani na wabunge   kutekeleza ahadi zao  walizowaahidi  wananchi   kwani  umesalia  mwaka  mmoja pekee wa kukamilisha  ahadi hizo  ili kujijengea  imani   kwa wananchi.  
Na EMMANUEL TWIMANYE

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.