AKUTWA AKIWA AMEJINYONGA HUKU CHANZO CHAKE KIKIWA HAKIFAHAMIKI HALMSAHAURI YA BUCHOSA

Mtu mmoja mkazi wa kitongoji cha Nyanzimilile kijiji cha Nyakabanga kata ya Lugata Halmashauri  ya  Buchosa  wilayani Sengerema amekutwa  juu ya mti  akiwa   amejinyonga hadi  kupoteza maisha   nje kidogo ya familia yake huku chanzo cha kifo chake kikiwa hakijafahamika.

Akizungumza na Radio Sengerema kwa njia ya simu Afisa Mtendaji wa kijiji cha Nyakabanga bw Bakari Matugunda amekiri kutokea  kwa  tukio  hilo  huku akimtaja  marehemu  huyo  kuwa  ni  Furahisha  Mtabuza mwenyeji  wa  kijiji  cha  Nyakabanga  (55)

Bwn,Matugunda ameongeza  kuwa  mtu  huyo  amepatikana  baada  ya  wananchi  kualikana  na  kuanza  kumtafuta, ndipo  walipomkuta  amejinyonga  katika  kitongoji  jirani  cha  Igoma ndani  ya  kata  hiyo,  hali  iliyozua  taharuki  kubwa  kwa  wananchi.


Katika  hatua nyingine   Afisa  huyo  amedai  kuwa  hatua  za  kuutoa  mwili  wa  marehemu  bado wanalisubiri  jeshi  la  polisi kwa  uchunguzi  zaidi,na kusema  kuwa  marehemu ameacha mke  na  watoto  6.

Na TUMAIN JOHN.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.