WATUMISHI WA AFYA WANAOTOA LUGHA CHAFU KWA WANGOJWA KUKIKONA CHA MOTO WILAYANI SENGEREMA .

Mganga mkuu wa wilaya ya  Sengerema   Dkt,  Peter Mahu amewaonya vikali   baadhi ya watumishi wa  zahanati na vituo vya afya wilayani Sengerema wanaotoa lugha chafu kwa wagonjwa pindi wanapokwenda  kufuata  huduma ya matibabu katika vito  vyao.

Kauli ya mganga mkuu imekuja baada ya   Radio sengerema hivi karibuni kutembelea zahanati ya Ngoma A  na  kupokelewa na malalamiko ya wananchi wa eneo hilo  wakiwatupia lawama waunguzi wa zahanati hiyo kwa kutoa lugha chafu kwa wagonjwa.

Hata hivyo  Dkt, Mahu amewaomba wananchi  kuendelea kutoa taarifa   kwa wahusika pindi wanapokutana na kauli chafu  kwenye  vituo  vya afya ama Zahanati  ili watumishi hao  wachukuliwa hatua kali za kinidhamu.

Said  Mahera.                                     

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.