UONGOZI WA RADIO SENGEREMA WALAANI VIKALI KUTUMIKA AMBAVYO SIVYO KATIKA JAMII

Uongozi wa  Kituo  cha habari na mawasiliano Sengerema Telecentere  umelaani vikali  wimbi la waandishi wa habari katika jamii   wanaotumia  jina la Radio Sengerema  kutafuta  habari wakati  si waandishi wa habari wa kituo hiki.   
SENGEREMA FM
Kauli hiyo imetolewa na  Meneja  mkuu  wa  Radio Sengerema  Bwn,Sostenes Tangaro   ambapo  amesema kuwa  mtu yeyote atakayebainika   kufanya  hivyo    hatua kali za kisheria  zitachukuliwa dhidi yake.

Hatua  ya uongozi wa Radio Sengerema kulaani vikali   suala hilo  imekuja  baada ya  baadhi ya  watu kutumia mwavuli wa Radio Sengerema kutafuta habari katika  jamii na kuwadanganya  kuwa ni waandishi wa habari  wa kituo hiki  kwa muda mrefu .   

Na Emmanuel Twimanye.


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.