ZOEZI LA UPIMAJI SHIRIKISHI WA VIWANJA WATARAJIWA KUANZA.
Related image

Zoezi la upimaji shirikishi wa viwanja wilayani Sengerema linatarajia kuanza rasmi mapema wiki hii katika Kata ya Mwabaluhi  wilayani Sengerema
Akizungumza na Radio Sengerema baada ya mkutano wa hadhara uliofanyika katika mtaa wa Kanyamwanza Kata ya Mwabaluhi wilayani Sengerema,Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni GEOID GEOMATICS  INTEPRISES Bwn Wadson Mwakalila,amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo.

Hata hivyo ameongeza kuwa endapo kamati iliyoteuliwa na wananchi pamoja na kampuni itathibitisha kuwa mmiliki wa kiwanja hana uwezo wa kulipia,kampuni itapima eneo bila malipo.

Nae diwani wa Kata ya Mwabaluhi Mh.Alex Kiganga,amesema kuwa zoezi hilo litakuwa na faida kubwa kwa wananchi na hivyo wajitokeze kwa wingi.


Kwa upande wao wananchi wameshukuru ujio wa kampuni hiyo na kuwaomba waitishe mkutano mwingine kwa ajili ya kuwapatia elimu  juu ya jambo hilo.
Na Michael Mgozi.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.