WIMBI LA  WATOTO  KWENDA  MACHINJIONI  KUOKOTA KITOWEO CHA NYAMA NA KUACHA KWENDA SHULE  HATIMAE LATATULIWA WILAYANI SENGEREMA.
Image result for kitoweo cha nyama
Baada ya Radio Sengerema kurusha habari inayohusiana na wimbi kubwa la watoto kwenda kuokota kitoweo cha nyama  katika machinjio ya  yaliyopo kata ya Nyatukara wilayani Sengerema na kushindwa kuhudhuria masomo shuleni tatizo hilo limekwisha.

Hayo yamebainishwa na Mkaguzi wa nyama wilaya ya Sengerema Bwn MORIS NDIHO amesema kupungua kwa suala hilo ni kutokana na sheria iliyopo kwa hivi sasa ambapo bila leseni hurusiwi kungia machinjioni.

Hata hivyo amesema mtu yeyote atakaeingia katika machinjio hayo atachukuliwa hatua za sheria ikiwa ni pamoja na kulipa faini ya shilling laki mbili ama kifungo cha miezi sita jela.

Aidha watu wanaoruhusiwa kuingia katika eneo hilo ni wale ambao wamepima afya zao asiwe na magonjwa ya kuambukiza kama kifua kikuu ambayo yanaweza kuwa hatarishi katika kitoweo cha nyama.

Na Deborah Maisa

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.