WAZAZI WATAKIWA KUWASAIDIA WATOTO KUFIKIA NDOTO ZAO ZA KIELIMU SENGEREMA

Wazazi wilayani Sengerema  mkoani Mwanza  wametakiwa kuacha kupuuza ndoto za watoto wao pindi wanapowaelezaa  ili kufikia malengo yao.
Hayo yameelezwa  na baadhi ya watoto walipokuwa  katika kipindi cha ulimwengu wa watoto kinachorushwa kupitia Radio Sengerema  ambapo wamedai kuwa wanapenda ndoto zao zitimie  ili wafanikiwe katika maisha yao ya baadae.

Nao  baadhi ya wazazi wamesema kuwa watoto ni taifa la kesho hivyo  wanatakiwa kuwasaidia ili wafikie malengo yao.


Sambamba      na hayo  wazazi  wamewaomba walimu wawe na ushirikiano  kwa wazazi, pamoja na   wanafunzi wazingatie wanayofundishwa shuleni ili waongeze ufaulu wao.


Aidha watoto hao wamewataka  wazazi kuwa ugumu wa maisha isiwe sababu ya kukwamisha ndoto zao. 

Na Glorius Balele.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.