MIGUU KIFUNDO SIO ULEMAVU KWANI UNATIBIKA

Wazazi na walezi wilayani Sengerema  mkoani Mwanza wameombwa kuwapeleka  watoto wenye matatizo ya miguu kifundo katika vituo vya afya ili wapatiwe  matibabu mapema kwani hali hiyo inatibika.

Hayo yamesemwa na Bwn..Chares Gabriel Mtaalamu Wa Tiba ya Mazoezi ya Viungo katika hospitali teule ya wilaya ya  Sengerema ambapo amesema kuwa ni vyema wazazi wa watoto wenye matatizo hayo wafike katika matibabu mapema  ili  watibiwe  kwa  wakati.

Mtaalam Gabriel amesema kuwa ni vyema kuzingatia maelezo ya wataalamu wanayopatiwa ikiwa ni pamoja na kuhudhuria mazoezi ya mara kwa mara kwani  ni mojawapo  ya  matibabu.

Hata hivyo amewataka wazazi kuwa na mwitikio katika kupata huduma hiyo kwa watoto wenye matatizo ya miguu kifundo ili waondokanena hali hiyo.

Na Glorius Balele

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.