SIKU YA MAADHIMISHO YA WATOTO NJITI DUNIANI

Jamii  imetakiwa kufahamu uwepo wa watoto njiti katika jamii na kwamba inatakiwa kuwathamini na kuwahudumia katika mahitaji yao muhimu.

Hayo yamesemwa na Mtaalamu wa kitengo cha watoto njiti Bi.Jesca Mgangara   wa hospital teule ya wilaya ya Sengerema katika  siku ya kilele ya maadhimisho ya mtoto njiti duniani ambapo amesema kuwa jamii haitakiwi kuwatelekeza wazazi wenye watoto njiti .

Bi .Mgangara amebainisha sababu zinazopelekea kuzaliwa mtoto njiti ikiwa ni pamoja na magonjwa kwa mama mjamzito na kufanya kazi ngumu wakati wa ujauzito.


Kwa upande wao wazazi wenye watoto njiti wamezungumza na Radio Sengerema jinsi wanavyokabiliwa na changamoto ya  kuwalea watoto njiti kukosa ushirikiano kwa baadhi ya wananchi. 
Na Shida Mabula.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.