WASHAURIWA KUZINGATIA SUALA LA USAFI WA MAZINGIRA.
Image result for picha ya usafi wa mazingira
Wananchi mkoani dodoma wameshauriwa kuzingatia suala la usafi ili kuepukana na magonjwa yanayoweza kujitokeza hasa magonjwa ya mlipuko.
Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa kamati ya usafi mtaa wa makongoro manispaa ya dodoma, bwana Kedmon nyongoto, wakati akizungumza na maisha fm, ikiwa ni katika kutekeleza rai iliyotolewa na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mhe dkt john pombe magufuli ya kila jumamosi ya mwisho wa mwezi kufanyika usafi wa mazingira nchini.
Kwa upande wake Paul elibariki mbaga ambaye ni mkereketwa wa mazingira amesema kuwa kwenye mtaa wa makongoro kuna kikundi husika ambacho kinahusika na kukusanya taka na kuzipeleka sehemu maalumu iliyotengwa na kata kwaajili ya kutupa taka.
Aidha baadhi ya wananchi wa mtaa wa makongoro wamesema suala la usafi linamuhusu kila mwananchi hivyo wanatakiwa kuwa na ushirikiano ili kuweka mazingira safi na kutoa wito kwa serikali kuweka njia mbadala ya matumizi ya mifuko ya nailoni kwani imeonekana kuwa uchafu kwenye mazingira.

Sambamba na hayo mwenyekiti wa mtaa wa makongoro amesema wamejiwekea utaratibu wa kulipa faini ya shilling elfu 50 kwa wale ambao hawatajihusisha na suala la usafi, mtu huyo atakamatwa na kupelekwa ofisi ya mtendaji kwaajili ya kuwajibishwa.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.