WANANCHI WA MWANGIKA WILAYANI SENGEREMA WAIOMBA SERIKALI KUCHUNGUZA MCHWA UNAOSHAMBULIA PESA ZA MAENDELEO

Wananchi wa kitongoji cha Mwangika Senta kilichopo kijiji cha Mwangika  katika kata Bangwe Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema wameiomba Serikali kufanya uchunguzi wa matumizi ya fedha zinazochangwa na wananchi kwa ajili ya shughuli za maendeleo katika kijiji hicho.

Image result for PICHA YA MKUTANO KATIKA HALMASHAURI BUCHOSA
Wakizungumza na Radio sengerema kwa nyakati tofauti wamesema  kuwa mwaka 2015 Mbunge wa jimbo la Buchosa Dr,Charles John Tizeba ambaye pia ni Waziri wa kilimo, amewahi kukabidhi pampu ya maji kwa ajiri ya kisima chenye kina kirefu, ilikukabiliana na changamoto ya maji  ambayo  imekuwa ikiwakabili wana nchi wa kitongoji hicho kwa muda mrefu.
Adha ya maji katika kitongoji mwangika senta  imekuwa ikiendelea kujitokeza huku wananchi wakiwa na sinto fahamu kuhusu fedha ambazo wamechanga kwa ajili ya kuchimbaji wa  kisima tangu mwaka 2015 walipo changa  fedha hizo na kulaani ukimya wa serikali ya kijiji kushindwa kuwasomea taarifa ya mapato na matumizi ya fedha hizo.
                                     
Radio sengerema imemtafuta mwenyekiti wa kitongoji hicho lakini jitihada za kumpata hazikufanikiwa, hali ambayo ikalazimika kumtafuta Mwenyekiti wa kijiji kuzungumzia hali hiyo.
Jumla ya watu miasita wamena kabiliwa na adha ya maji katika Kitongoji hicho hali ambayo huwalazimu kufuata huduma hiyo umbali mrefu nyakati za usiku hususani kipindi cha kiangazi.

Na Katemi Lenatus


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.