WALIMU WANACHANGIA  CHOO KIMOJA NA WANAFUNZI.
Image result for PICHA YA CHOO
PICHA KUTOKA MTANDAONI
Walimu    wa shule ya msingi  Lugasa  kata ya Nyakaliro Halmashauri ya Buchosa  Wilayani Sengerema   Mkoani Mwanza  wamelazimika kuchangia choo kimoja na wanafunzi  wao kutokana na upungufu  wa matundu ya vyoo shuleni hapo.

Hayo yamebainishwa na Mwl, mkuu wa Shule ya msingi Lugasa  Experansia Malila alipokuwa akizungumza na Radio Sengerema Ofisini kwake amesema, shule hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa matundu ya  vyoo  kwani matundu yaliyopo ni saba  na hayawezi kumudu idadi ya wanafunzi hao.

Nao   walimu wa shule hiyo wamesema hawajisikii vizuri kitendo cha  kuchangia choo kimoja na wanafunzi wao kwani itapelekea chanzo cha kuporomoka kwa maadili  shuleni  hapo.
Kwa upande wao wanafunzi wa shule ya msingi Lugasa wameiomba jamii na serikali kwa ujumla iwatazame kwa jicho la tatu ili kuwanusuru na changamoto hiyo.

Aidha Mwl Mkuu  wa shule hiyo ameiomba jamii walichukue swala hili kama tatizo la kwao na siyo  Kuiachia   serikali  pekee.

Na WINFRIDA NGASSA       

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.