WALIMU WALALA NJE KWA MIUJIZA WILAYANI SENGEREMA

Image result for picha ya kibuyu cha mganga na mkia wa ng'ombe
Walimu saba wanaofundisha Shule ya Msingi Soswa Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema wamejikuta wamelala nje pamoja na familia zao huku wawili kati yao wakiwa wamenyolewa nywele kichwani na sehemu za siri.
Mwalimu wa Shule ya Msingi Soswa, Petro Lukas amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamukia novemba 15 mwaka huu  wakati walimu hao walipokuwa wamelala ndani ya nyumba zao ndipo walipotahamaki usiku wakijikuta wamelala nje.
Amesema asubuhi kulipopambazuka walimu hao wamezinduka na kutoamini kilichotokea kwani walipoingia ndani ya nyumba zao wamekuta damu zimetapakaa chumbani na sebuleni pia vibuyu vikiwa vimevalishwa shanga nyeupe vikiwa kitandani na chini kitendo hicho kimewafanya waombe msaada kwa jamii inayowazuguka.
Mwalimu Lukas amesema kati ya walimu hao wawili wameathirika zaidi na tukio hilo kwa kupata mshituko ambapo mmoja amenyolewa nywele kichwani huku mwingine akinyolewa nywele sehemu za siri.
Kutokana na mshtuko huo mwalimu mmoja amepelekwa kituo cha afya cha Mwangika kwa matibabu na mwalimu mwingine anaendelea na matibabu na kwamba hali zao zimeelezwa kuwa zinaendelea vizuri.
Mganga Mkuu Halmashauri ya Buchosa, Dk Ernest Chacha amekiri kumpokea mwalimu mmoja kati yao katika kituo cha afya Mwangika na kwa sasa anaendelea kupatiwa matibabu na baada ya uchunguzi wa kitaalamu kukamilika watatoa taarifa.

 

 


Na Veronica Martine

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.