MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI ITAFUTIWE SULUHU YA KUDUMU

Wakulima    wa   mtaa  wa  kilabela   kata  ya  Mwabaluhi  wilayani  Sengerema  mkoa  wa  Mwanza, wametakiwa  kuwa na  ushirikiano   na  wafugaji  hususani   katika  msimu  huu  wa  kilimo  ili   kuepuka  kutokea  migogoro  dhidi  ya  wakulima  na  wafugaji.
Image result for PICHA YA MIFUGO
Kauli hiyo  imetolewa  na   mwenyekiti  wa  mtaa  huo  Bwn,  Samweli   Macheni  Nzungu   ambapo  amesema  kuwa    kuna   wafugaji  wanaotaka  kuvuruga  amani  mtaani  humo kutokana  na  kutoa  kauli  chafu  pindi   mifugo yao inapoharibu    mazao  ya  wakulima.

Bwn,  Nzungu  ameeleza  kuwa  mpaka  sasa  amesha  pokea  kesi  nyingi  kutoka  kwa  wakulima  na  wafugaji  na  ndani  ya  kesi  hizo  zipo zilizo  tatuliwa bila  kufika  ofisini  kwake  na  mbili  zimetatuliwa ofisini hapo  bila kuwa  na  shida yoyote kutokana  na  uelewa  wa  baadhi  ya  wafugaji.

Aidha  Mwenyekiti  huyo     amewaomba   wakulima  na wafugaji  wa  mtaa  wake  kuachana  na  malumbano  yasiyo na tija   na   badala  yake  waungane  pamoja  ili  kupata maendeleo ya  mtaa,na  wilaya  ya  Sengerema  kwa  ujumla

Na Thobias Ngubila

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.