WAHOFIA KUKUMBWA NA UGONJWA WA KIPINDU PINDU.
Image result for picha ya usafi wa mazingira  
Baadhi ya    Wananchi  Wilayani Sengerema   Mkoani Mwanza Wamelalamikia  suala    la       kutozolewa  kwa   taka  zilizojaa kwenye vizimba  kwa muda mrefu  huku Mamalaka husika  zikilifumbia macho suala hilo.      
Wakitoa  Malalamiko  hayo   wananchi  hao  wamesema    wamekerwa  na  harufu     mbaya  kutoka  kwenye vizimba hivyo    kwani  uchafu    haundolewi kwa wakati  huku wakihofia kukumbwa na magonjwa ya milipuko ikiwemo kipindupindi katika msimu huu wa mvua zinazoendelea kunyesha.     
Radio   Sengerema  imezulu katika  katika viunga mbalimbali vya mji wa sengerema  ambavyo  vinalalamikia kutozolewa taka kwa wakati   ambapo     baadhi  ya  wananchi   wamepasa kilio chao  kuwa  licha ya kutozwa ushuru wa taka lakini taka hizo hazizolewi. 
Maelezo  ya  wananchi  yamenifanya niwatafute  wafanyakazi  katika kampuni  ya   STUMACORT   COMPANY   LIMITED  ambao  pia  wamesema  kuwa  tatizo  la  usafi  kutofanyika  kwa  wakati  ni  wao  kutolipwa stahiki  yao  kwa  muda  wa  zaidi  ya  mwezi  mmoja.

Kwa  upande  wake Meneja   wa   kampuni  ya  STUMACORT   COMPANY   LIMITED   Bwn,Charles  Ngaiza  amekiri  kuwepo   kwa  deni  la  wafanyakazi  analodaiwa kiasi cha fedha  shilingi milioni  5 laki sita     huku  akiri pia   kutozolewa  uchafu   uliojaa kwenye vizimba    kwa  wakati  mwafaka  na  kuongeza  kuwa   ni kwa sababu ya   ofisi  yake  kutokuwa  makini    katika  usimamizi  wa  ukusanyaji  wa  mapato jambo ambalo  limepelekea   kushindwa   kumudu kulipa  stahiki  za   wafanya   usafi.


Sanjari  na  hayo  Bwn, Ngaiza   ameongeza   kuwa   kampuni  yake  imekuwa  kwenye   mkataba  na  Halmashauri ya  Sengerewma   kwa  muda  wa   miezi  mitatu  ambapo mkataba  huo  umeisha   01.11.2017 , na kwamba  halmashauli  imetoa  matazamio  ya  mwezi  mmoja  tena kutokana  na  kampuni  kuonekana  kuwa  na  changamoto  nyingi  ambazo zimekuwa  zikiikabili .     

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.