VIJANA KATA YA KASUNGAMILE WILAYANI SENGEREMA WATAKIWA KUFANYA KAZI

Vijana  wa  kata  ya Kasungamile Wilayani Sengerema  Mkoani  Mwanza  wametakiwa  kulima zao la pamba ili kuongeza  mapato yao kiuchumi  na kuacha kukaa vijiweni katika kipindi hiki cha kilimo.


Hayo yamebainishwa na Diwani wa  kata ya  Kasungamile Mh, Julias Mussa Ndekeja wakati akizungumza na Radio Sengerema ofisini kwake amesema kulima zao la pamba kutawasaidia vijana kuongeza kipato na kupata mitaji itakayowaendeleza kimaisha.


Mh, Ndekeja ameongeza kuwa hakuna haja ya vijana  kuilalamikia Serikali   kwa kukosa fursa za ajira katika kipindi hiki cha masika badala yake wanatakiwa wajiajiri kupitia kilimo.

Diwani huyo amewatahadharisha vijana wanaopenda kukaa vijiweni wakati wa kazi waache mara moja na badala yake wajishughulishe kufanya kazi.

Ameongeza kuwa ikiwa wananchi pamoja na viongozi watasimamia vyema ufufuaji wa zao la pamba kuna matumaini makubwa ya zao la pamba kuwa na mavuno mazuri Kutokana na hali ya hewa inavyoendelea.

Na Charles  Sungura 

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.