UNESCO  WALETA MWAROBAINI  WA MTOTO WA KIKE KUFIKIA NDOTO ZAKE ZA KIELIMU WILAYANI SENGEREMA.
Related image

Mafunzo yaliyofanyika kwa  muda  wa  siku  nne  yaliyolenga  kuutambulisha  mradi  wa kuwawezesha  watoto  wa kike kufikia ndoto zao za kielimu yamemalizika  Novemba  9 mwaka  huu.
Akifunga mafunzo hayo  mtalaamu  wa Elimu  na  Afya wa shirika  la  umoja wa  mataifa linalojishughulisha na  utoaji wa   Elimu,Sayansi  na  Utamaduni ( UNESCO)  Mathias  Hermani    amewashukuru  washiriki  wote  na  kuwaomba  wautekeleze  mradi  huo kwa  nguvu  zote  kwa  sababu unalenga  kuinua  maisha  ya  mtoto  wa kike.

Akizungumza  kwa  niaba  ya  Mkurugenzi  Mtendaji wa halmashauri  ya  Sengerema    Afisa  elimu  wa  shule  za  sekondari  wilayani  Sengerema  Godwini  Balongo amewashukuru  watumishi  wote  waliohudhuria  semina  hiyo  na kuahidi  watayafanyia  kazi  yale  walioelekezwa.

Kwa  upande  wake  mkuu  wa  shule  ya  sekondari  Ngweli  Gibson  Dobele ambaye  ni  mmoja  wa  washiriki  wa  mafunzo hayo  na  pia  shule yake  ni moja  kati  ya  shule  ambazo  zitafikiwa  na  mradi  huo  amesema  endapo  mradi  huo  utatekelezwa  ipasavyo  utasaidia  kupunguza  mimba  kwa  wanafunzi.

Hata hivyo  amesema  kuanzishwa  kwa  mradi  huo  kutaongeza  uwezo  wa  kitaaluma  kwa  wanafunzi  wa  kike  endapo  watajitambua.

Na Neema Hussein

                                             

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.