MVUA YAHARIBU HEKALI 47 ZA MAHINDI NGOMA WILAYANI SENGEREMA




Zaidi ya hekali 47 za mazao  ya  mahindi katika kata ya Ngoma wilaya ya Sengerema  mkoani Mwaza zimeharibiwa na mvua ya mawe     iliyoambatana  na upepo  mkali.       

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Afisa ugani wa kata hiyo Bw,STANLEY SHIJA ameiambia radio sengerema  kuwa mazao  yaliyoharibiwa ni pamoja na   mahindi  mhogo,maharage  na mtama. 

Ameyataja  maeneo  yaliyokubwa  na   tukio hilo kuwa  ni pamoja na kijiji cha Lubungo ,na Nyabila  na  kuwaomba wakulima kufanya utaratibu wa kupanda mazao mapya haraka ili kuendana na msimu wa kilimo.


Hata hivyo  amewashauri   wakulima  wasisubiri   kupata pembejeo kutoka serikalini  pekee  kwani  watachelewa  kwenda na kazi ya msimu  wa kilimo   na  hivyo wanunue mbegu kwenye  maduka  ya   kilimo.
Na Anna Elias

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.