MKUU WA WILAYA  YA SENGEREMA  ATANGAZA VITA KALI KWA VIJANA  WASIOFANYAKAZI 
Image result for PICHA YA MKUU WA WILAYA YA SENGEREMA
EMMANUEL KIPOLE

Vijana wametakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kujikwamua kiuchumi na kuachana na dhana ya kukaa vijiweni nyakati za kazi hususani kipindi   hiki  cha    kilimo.
Hayoyamebainishwa na Mkuu wa wilaya ya Sengerema Mh.Emmanuel Kipole wakati akizungumza na vikundi vya vijana wilayani sengerema.
Mh.Kipole amesema kuwa,inasikitisha kuona vijana wakisubili kukimbizana na selikari   mitaani muda wa kazi,jambo  ambalo   hupelekea kuongezeka kwa vitendo vya kihalifu.

Mkuu wa Wilaya   amewataka  kuutumia ujana wao vizuri  pindi wanapokuwa na nguvu,kwani bila kujituma kipindi cha ujana hawataweza kumudu maisha yao uzeeni, kwani   vijana wanawajibu wa kujenga nchi  yao.

Hata  hivyo Mh,Kipole  ameshangazwa na vijana ambao hawajishugulishi  katika kazi yoyote  kwa kuwa wako    hatarini   kutumbukia  katika  makundi ya kihalifu  pamoja na  utumiaji wa dawa za kulevya,hali ambayo  itadidimiza uchumi  wanchi kwa ujumla.
Na Michael Mgozi.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.