MELI YAZAMA NA WATU 17 WAOKOLEWA NDANI YA ZIWA VICTORIA


Watu 17 wameokolewa baada ya meli ya MV Julius kuzama ziwa Victoria usiku wa kuamkia novemba 16 ikiwa na watu pamoja na mizigo, kilomita chache kutoka kisiwa cha Goziba Wilayani Muleba Mkoani Kagera.


Meli hiyo inayofanya shughuli zake za usafirishaji kati ya Mwanza na kisiwa cha Gozba Wilayani Muleba Mkoani Kagera, ilizama  ikiwa na nahodha, wabeba mizigo pamoja na mzigo wa magunia 750 ya dagaa.



Jeshi la Polisi linaendelea kufuatilia kubaini kama kuna waliosahaulika majini, na taarifa zaidi zitatolewa baada ya zoezi hilo kukamilika.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.