MATUMAINI YAJA KWA WANANCHI BAADA YA KUANZA KWA UPANUZI WA ZAHANATI KUWA KITUO CHA AFYA

Wananchi wa kitongoji cha Kasenyi ,kijiji cha Kasenyi kata ya Kasenyi wilayani Sengerema   wamekuwa na matumaini ya mwendelezo mzuri  wa upanuzi wa zahanati ya kijiji hicho kuwa kituo cha afya cha kata hiyo.

Akizugungumza na Radio Sengerema Mwenyekiti wa Kitogoji cha Kasenyi  Bwn,  Juma Ramadhan amesema kuwa upanuzi huo ni agizo la Rais wa awamu ya nne  DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE alipoagiza kila kata iwe na kituo cha afya.
BW RAMADHAN amesema kuwa wananchi wa kata hiyo wameitikia wito huo na kushiriki kikamilifu katika upanuzi wa zahanati hiyo kwani kukamilika kwake kutapungunza gharama ya kwenda katika hospitali teule ya wilaya Sengerema kwa ajili ya matibabu zaidi.

 Aidha mwekitikiti huyo amewaomba wananchi wa kijiji hicho kuendelea kujitolea katika upanuzi wa zahanati hiyo ili waondokane na adha wanayoipata.
Na Tumain John.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.