KAYA 762 ZAKABILIWA NA UKOSFU WA VYOO GEITA
Image result for PICHA YA CHOO
Jumla ya   kaya   762    zinakabiliwa na  ukosefu  wa  vyoo  katika  kata ya Bukwimba   Wilayani Nyang’hwale  Mkoani Geita .
Awali akitoa taarifa hiyo mbele ya kikao cha baraza la madiwani  Diwani viti maalumu  wa kata ya bukwimba Bi. GWIDO TANU amesema wakazi wa kata hiyo hawana mwamko wa kujenga vyoo vya kudumu hali  itakayopelekea   mlipuko wa magongwa ya mlipuko  hasa katika   kipindi hiki  cha  mvua zinazoendelea kunyesha.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri  ya Nyang’hwale Bw,CARLOS GWAMAGOBE amesema wananchi wanatakiwa kujua nyumba ni pamoja na choo hivyo serikali za vijiji katika kata hiyo wahamasishe ujenzi wa vyoo kwa sababu magonjwa yakitokea hayatachagua wenye vyoo na  wasiokuwa na vyoo.


Aidha jamii imetakiwa kutambua wajibu wake katika suala la usafi katika mazingira yanayomzunguka bila kusubiri  hadi  tamko la serikali.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.