KAMATI YA UPIMAJI WA ARDHI YAPEWA SEMINA

Image result for PICHA YA viwanja

Hatimae  zoezi  la  utoaji  Semina  wa  kamati  zilizoteuliwa  na  wananchi  kwa  ajili  ya  usimamizi  wa  upimaji shirikishi  wa  viwanja  katika  kata  ya  Mwabaruhi  wilayani Sengerema limekamilika.

Semina  hiyo imefanyika  katika  jengo  la  Ofisi  ya kata   ya  Mwabaruhi  kwa  lengo  la  kuchagua viongozi  wa  kamati  kutoka   mitaa  hiyo  miwili  ya  Kanyamwanza  na  Ofisini katika kata hiyo.

Akitoa  semina  hiyo Mkurugenzi  wa  kampuni  ya  upimaji  ya Geoip Geomatic  Enterprises  Bwn, Watson  Mwakalila  amefungua  semina  kwa  kuwashukuru  wanakamati  kwa  mahudhurio  yao  mazuri na  kuwataka  kuchagua  viongozi  watatu  kwa  kila  kamati kutoka  kwenye kamati  zote  mbili zilizo kuwa  kwenye  semina  hiyo.

Kwa upande  wao  wanakamati  katika  semina  hiyo  wameonekana  kufurahishwa  na  semina  hiyo  na  kuteua   wajumbe  watatu  kwa  kila  kamati  ambapo  kamati  ya  mtaa wa  Kanyamwanza  mwenyekiti  Revocatusi  Marosha,katibu Joseph  Max  Kayanda  na  mhasibu  ni Oriva  John,vilevile  kamati  ya  Ofisini  mwenyekiti  ni  Velitatis  Max,katibu Hatari Erasto  na  mhasibu  ni  Getruda  Nestory.


Aidha  wanakamati  hao  kupitia  semina  hiyo  wamewaomba  wananchi   kutambua  umuhimu  wa  hati  miliki  na kwamba  kupitia  hilo  sasa  wanayofursa  ya  kumiliki  maeneo  tofauti  na  ofa  za  viwanja  zilizokuwa  zikitolewa  awali.

Na Thobias Ngubila

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.