KAMATA KAMATA YA MIFUGO KUENDELEA NCHI NZIMA

Image result for PICHA YA MIFUGO

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdalah Hamis Ulega amesema serikali haitasita  kukamata mifugo itakayoingia nchini bila kibali ikitokea nchi jirani.

Naibu waziri ameyasema hayo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Ngara mkoani Kagera Mh,Alex Raphael Gashaza ambapo alitaka kujua jimbo la Ngara linamifugo mingi ikiwemo ng’ombe pamoja na mbuzi je ni lini serikali itachimba marambo ya kunyweshea mifugo.

Akajibu swali hilo naibu waziri amesema wilaya ya Ngara kuwa na Mifugo mingi inasababishwa na kuingizwa mifugo kutoka nchi jirani bila kufuata utaratibu zilizopo.



Hivi karibuni waziri wa mifugo na uvuvi LUHAGA MPINA alitangaza kupiga mnada ng’ombe zaidi ya 10,000 wa nchi za Uganda na Rwanda waliokatwa katika oparesheni inayoendelea nchini. 
Na Deborah Maisa

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.