HUDUMA YA MAMA WAJAWAZITO NA WATATO YAFANIKIWA KWA KIASI KIKUBWA SENGEREMA.

Imeelezwa kuwa Elimu inayotolewa kwa wananchi juu ya afya ya uzazi pamoja na huduma ya afya kwa watoto walio chini ya umri wa miaka 5 imewafikia wananchi na kuwa  na mafanikio mazuri kwani  watoto idadi yao kwa mwezi ni 975 na akina mama wajawazito ni zaidi ya 200.

Hayo yamebainishwa na Dkt.NELLSON MTABILWA  ambaye ni  Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya wilayani Sengerema wakati akizungumza na Radio Sengerema.


Pia Dkt.MTABILWA amesisitiza kuwa kutokana na elimu wanayopatiwa ni vyema waendelee kuizingatia ili kuimarisha afya zaidi na kuepusha vifo kwa watoto wenye umri mdogo na kwa akina mama wajawazito.


Mganga Mfawidhi amewaomba wazazi pamoja na walezi wale waliopata elimu juu ya afya ya uzazi pamoja na huduma ya afya kwa watoto wenye umri mdogo wawe mabalozi kwa wengine.

Na Glorius Balele

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.