ELIMU JUU YA UPIMAJI WA VIWANJA SENGEREMA

Wananchi  zaidi   ya  mia  mbili  wamepatiwa    elimu   juu   ya  upimaji  wa viwanja  katika  mtaa wa kisima  cha  chumvi  kata ya  Nyatukala  wilayani  sengerema  mkoani mwanza.
Related image
Elimu  hiyo  imetolewa na mkurugenzi wa  kampuni   lisilokuwa la kiserikali la upimaji  wa  viwanja  bwana,WATTSON   MWAKALILA     katika  mkutano  mkuu  uliofanyika  katika  eneo  la kisima cha chumvi  kata ya nyatukala wilayani sengerema.
MWAKALILA amesema   kuwa hali hiyo   imekuja   kutokana  na tamko  la    Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania     Dkt,  John Pombe Magufuli   kwa  kushirikiana  na waziri  wa ardhi  nyumba na maendeleo ya makazi    Mh, WILLIMU  LUKUVI    kufikia  mwaka  2020  Tanzania  iwe imetoa  hati  kuanzia  laki nne  na  kuendelea.

Pia  amesema  kuwa  makampuni  takiribani  58   hapa  nchini  yameombwa  kutembelea  halmashauri  na  manisipaa          na  kupanga  bei  elekezi  ambayo   itawasaidia     wananchi   kufanikisha  shughuli  ya upimaji  wa  viwanja.

Kwa  upande  wake   kaimu  mkurugenzi  Mtendaji   wa halmashauri  ya  wilaya  ya  sengerema  Bi, LILIAN  KAIZA  amesema kuwa  kwa sasa kuna makampuni  manne  ambayo  yamefika  katika  halmashauri  ya  wilaya  ya  sengerema  kwa ajili  ya kutoa  elimu  hiyo  ya upimaji wa  viwanja.

Nao   baadhi  ya  wananchi  wamedai  kulipwa  fidia  endapo  kama  mwananchi  ataamuliwa    kubomoa  nyumba  yake  na  kupisha  barabara  za  mitaa  hiyo.

Aidha  katika  hatua  nyingine  B,LILIAN    amesema  kuwa  hivi  karibuni  wananchi  wataanza  kulipa  kodi  za  majengo  kwa wenyeviti  wa  vitongoji  ili  kuondoa  usumbufu  waliokuwa  wakiupata  hapo   awali ili kuondoa msongamano wa wananchi  katika halmashauri  hiyo.

Na Enosy Mashiba

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.