CHANGAMOTO WANAZOKUMBANA NAZO WAJASILIAMALI WADOGO WADOGO JIJINI MWANZA.

Wajasiriamali mbalimbali wenye viwanda vidogo vidogo mkoani mwanza wameelezea changamoto mbalimbali zinazowakwamisha kukuza soko la bidhaa zao  ikiwemo ya kutokuwa na uwezo wa kuthibitishiwa  bidhaa zao na TBS pamoja  TFDA hali inayowakwamisha  kukuza soko la  biashara zao.

Wakizungumza katika kampeni ya  amsha viwanda iliyoandaliwa na shirika la sido kwa kushirikiana na tiled inayofanyika wilayani nyamagana jijini mwanza wamesema kuwa wamekuwa wakitengeneza bidhaa zao nzuri lakini wamekuwa hawafikii malengo kutokana na bidhaa hizo zianakuwa hazijathibitishwa na mamlaka hizo kutokana na gharama kuwa kubwa ambapo wameiomba serikali kuwasaidia suala hilo

Akizungumzia kampeni hiyo  meneja wa sido mkoani mwanza  bakari songwe  amesema kuwa lengo la kampeni hiyo ni kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wanachi walioanzisha viwan da vidogo vidogo na ambao bado ili waweze kufikia malengo na kuendena na tanzania ya viwanda


Aidha msimamizi mkuu wa mradi wa kuwaendeleza wajasiriamali tanzania tled Frank Jirabi amesema  kuwa kampeni hiyo inatarajia kuwafikia wajasiriamali 1,760 nchi nzima lengo kubwa ikiwa ni kuwafikia wanawake.

Na Said Mahera

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.