ANUSURIKA KIFO KWA AJALI YA PIKIPIKI WILAYANI SENGEREMA

Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la JEREMIA COSMAS mkazi wa Bukala wilayani Sengerema  amenusurika  kifo    baada  ya kugongana  na gari aina ya probox yenye namba za usajili T 664 DHT katika makutano ya barabara ya Kamanga na Busisi wilaya Sengerema   Mkoani   Mwanza.

Ajali hiyo imetokea baada ya dereva wa pikipiki kuingia katika makutano ya barabara ya kamanga na busisi akitokea barabara ya misheni na kugonga ubavuni mwa gari lililokuwa  likitokea barabara ya Geita.

Mganga mkuu wa hospitali teule ya wilaya ya Sengerema Dkt.Mary Jose amethibitisha kupokea majeruhi huyo na hadi Radio Sengerema inaondoka katika chumba cha dharula hospitalini hapo mgonjwa alikuwa anaendelea na matibabu. 

Jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani limefika katika eneo la tukio na kuchukua taratibu za awali kwa mjibu wa sheria.

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.