Waziri Mkuu wa Tanzania Mh Kassim Majaliwa amewataka Maafisa watendaji wa mikoa yote nchini kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya viwanda katika maeneo yao kwani  vitasaidia katika kutatua tatizo la ukosefu wa ajira hususani kwa vijana.
SULUHU LA UKOSEFU WA AJIRA KWA VIJANA YAPATIKANA
 Image result for picha ya waziri mkuu kasimu majaliwa
Waziri Mkuu ameyasema hayo wakati alipozungumza na Maafisa watendaji na wananchi wa mkoa wa Morogoro ambapo amesema mpango wa Serikali wa kujenga uchumi wa viwanda ambao unalenga kuinua uchumi wa Taifa kutoka wa chini kwenda uchumi wa kati, hivyo ni muhimu kuvifuatilia.

Waziri Majaliwa ameongeza kwamba muda mrefu sekta ya viwanda nchini imekuwa haifanyi vizuri jambo ambalo limesababisha kuongezeka kwa tatizo la ajira na mazao yalikosa soko.

Hata hivyo Waziri Mkuu amesisitiza uaminifu kwa wafanyakazi walioajiriwa katika viwanda mbalimbali kuwa waaminifu ili kuviwezesha viwanda hivyo kuendelea na uzalishaji.


Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.