WATAKAOIBA MITIHANI KUBURUZWA MAHAKAMANI
Image result for PICHA YA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA
Wanafunzi wa darasa la saba wakitarajiwa kufanya kufanya mtihani
Jumla ya  watahiniwa   Elfu nane  mia tano hamsini na moja   wanatarajiwa kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi  Wilayani  Sengerema  Mkoani   Mwanza .

Afisa elimu wa shule za  msingi  Wilaya  ya  Sengerema  Bwn,Oscar Kapinga  amebainisha kuwa kati ya watahiniwa hao   wavulana  ni  elfu nne mia moja thelathini  na nane  na wasichana ni elfu nne kumi na tatu .

Akizungumzia  suala la usimamizi wa mitihani hiyo Kapinga amesema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha  suala la udanganyifu wa kuiba  mitihani halitokei huku akiwatahadharisha wasimamizi na wanafunzi  watakaofanya  udanganyifu  wa kuiba mitihani hiyo  hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Hata hivyo afisa elimu amewataka wazazi na walezi  kutowashinikiza watoto wao kufanya vibaya mtihani hiyo kwa lengo la kushindwa kuendelea na masomo yao ya sekondari hapo baadae ili wawasaidie kazi za nyumbani pamoja na kuolewa ili  wapate mali.
Mitihani ya  kuhitimu elimu ya msingi inatarajiwa kuanza kufanyika  kesho  septemba 6 hadi  Septemba 7 mwaka huu nchini   kote.
Na,Emmanuel Twimanye.                

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.