WAPIGWA FAINI YA LAKI MOJA KISA LUGHA ZA UCHOCHEZI 
fedha ya Tanzania

Watu  wawili  wakazi  wa  mtaa wa Nyacheche Road kata ya Nyatukala Wilayani Sengerema wametozwa faini ya shilingi laki moja (100,000) kwa kosa la  kutoa lugha za uchochezi katika jeshi la jadi maarufu kama sungusungu.
Hayo  yamebainika  kwenye mkutano  mkuu  wa  sungusungu uliofanyika  katika  eneo  hilo  baada  ya  kusomwa  taarifa  ya  jeshi  hilo  na  katibu  wa  sungusungu  Sijali Ibrahimu.
 Baadhi  ya  wananchi  wamelaani  kitendo  hicho  na  kusema  kuwa ni  lazima  wachukuliwe  hatua  kali  kwani  jeshi hilo linafanya  kazi usiku  na  mchana  kuhakikisha  suala la ulizi na usalama  linazidi kuimarika.
Nao  viongozi   wa  sugusungu  waliokumbana  na  sakata  hilo wametaja  majina ya watu  hao ambao wanatuhumiwa kutoa lugha za uchozhezi.
Nae mwenyekiti wa kata ya Nyatukala bwn Pelana Bagume Wametaka wananchi kuachana na lugha za uchochezi kwa zinaweza kuwasabibishia matatizo makubwa hapo baadae.

Mkutano huo umehudhuliwa na zaid ya wananchi 181 pamoja na viongozi wa jeshi la jadi sungusungu kutoka vitongoji kata jirani.
Na Said Mahera

Comments

Popular posts from this blog

KISIWA CHA ZILAGULA KIPO HATARINI KUKUMBWA NA KIPINDUPINDU WILAYANI SENGEREMA

WANAFUNZI WAONDOKANA NA ADHA YA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA ELIMU KATIKA KIJIJI CHA ILEKANILO WILAYANI SENGEREMA.